Monday, 5 May 2014

Mwaikimba asema usingizi wake haupotezwi na Kavumbagu.



Mshambuliaji ngongoti wa Azam FC, Gaudence Mwaikimba, amesema usajili wa Mrundi Didier Kavumbagu haumnyimi usingizi hata kidogo kwani yeye ni mchezaji na anaijua kazi yake,imeripotiwa na Mwanaspoti.
Mapema wiki iliyopita, Azam ilimsainisha Kavumbagu mkataba wa mwaka mmoja kutoka Yanga, hivyo kuongeza ushindani wa namba kwenye safu ya ushambuliaji inayoundwa na washambuliaji; Kipre Tchetche, John Bocco, Brian Umony na Gaudence Mwaikimba.
Mwaikimba ambaye hata kabla ya ujio wa Kavumbagu hakuwa akipata nafasi kikosi cha kwanza licha ya kuchezeshwa kwenye mechi za mwishoni msimu uliopita, alisema ujio wa Kavumbagu utawaongezea nguvu kwenye safu ya ushambuliaji na yeye binafsi anaamini bado ana nafasi ya kukitumikia kikosi hicho.
“Kavumbagu ni mchezaji mzuri na hakuna mtu asiyejua uwezo wake hivyo mimi binafsi nimefurahi kwa sababu ni maendeleo kwenye timu hususani tunapojiandaa na maandalizi ya mechi za kimataifa mwakani,” alisema Mwaikimba aliyewahi kukipiga Yanga miaka ya nyuma.
“Lakini mchezaji mahiri siku zote haogopi ujio wa mchezaji mwingine, mimi ni mchezaji na ninaifahamu kazi yangu, nitajitahidi kufanya vizuri ili kushindana.”
Chanzo:Mwanaspoti.

0 comments:

Post a Comment