Pique ajifunga zaidi Barcelona,Sagna kuelekea Manchester city.
Usajili barani Ulaya umeendelea kuchukua nafasi yake ambapo hii leo kipa mkongwe wa AC Milan Christian Abbiati (pichani) ameongeza mkataba wa kuidakia klabu hiyo hadi mwakani Juni 30.Wakati jana Gerard Pique wa Barcelona ameongeza mkataba wa kuichezea klabu hiyo hadi mwaka 2019.
Beki wa kulia wa Arsenal,Bacary Sagna anajiandaa kusaini mkataba na Manchester City ambao utamfanya awe analipwa kiasi cha pauni laki 1 na efu 40 kwa wiki( £140,000).
Mfaransa huyo anamaliza mkataba na
washika bunduki na alionyesha dhairi kutotaka kuendelea kusalia Emirates
Stadium.
Klabu za Liverpool na Newcastle
United zipo katika mbio za kuwania saini ya kiungo wa West Ham,Mohamed Diame
Arsene Wenger anajiandaa kumnyakua
beki wa Toulouse,Serge Aurier ambapo ndiyo utakuwa uhamisho wake wa kwanza
kipindi hiki cha majira ya joto ili akazibe nafasi ya Bacary Sagna ambaye
anataraji kujiunga na Manchester City mara baada ya kombe la dunia.
Klabu ya Valencia ipo njiani
kutafuta mshambuliaji mpya majira ya joto na tayari wameonyesha nia ya kumtaka
nyota wa Benfica,Rodrigo
Newcastle
wana dhumuni la kupeleka ofa kwa kiungo wa Montpellier,Remy Cabella kabla ya
kuanza kwa michuano ya kombe la dunia.
Nyota
huyo mwenye miaka 25 yupo katika orodha ya wachezaji wanaoweza kuitwa baadae
kwenye kikosi cha timu ya Taifa ya Ufaransa na thamani yake inafikia Euro
milioni 10 huku Newcastle wakiwa wameandaa ofa ya Euro milioni 8.
Inter Milan wanatazamia uwezekano wa
kumnasa mchezaji wa Borussia Monchengladbach,Granit Xhaka majira haya ya joto
wakiwa na lengo la kuimarisha safu yao ya kiungo.
Roma wapo katika hali ya kumtaka
winga wa Porto,Juan Iturbe ambaye alicheza msimu wa mwaka 2013-14 kwa mkopo
katika klabu ya Verona na itawalazimu watoe kiasi cha Euro milioni 15 kwa nyota
huyo
Manchester
City na Newcastle United zimekiri kuwa katika mbio za kutaka kupata saini ya
beki wa kati wa Stoke City,Ryan Shawcross.
ia
Everton anajiandaa kumbakiza Lacina Traore kwa mkopo wa muda mrefu zaidi
klabuni hapo mara baada ya kumchukua mwezi Januari kutoka katika klabu ya
Monaco ya Ufaransa.
Imeandaliwa na mtandao huu kushirikiana na mitandao ya nje.
0 comments:
Post a Comment