Klose akifunga bao moja leo ataifikia rekodi ya Ronaldo
Michezo ya kombe la dunia inaingia siku yake ya 5 huku dunia leo ikisubiri mchezaji mkongwe wa Ujerumani Miroslav Klose kusawazisha rekodi ya ufungaji mabao tokea kombe la dunia lianze mwaka 1930 iwapo akifunga bao na itategemea kama akipangwa na kocha Joachim Loew katika mchezo utakaopigwa hapo baadaye Ujerumani na Ureno.Klose, mwenye miaka 36 mchezaji wa kihistoria aliyefunga mabao mengi kwa upande wa Ujerumani amefunga mabao 14 nyuma ya mshambuliaji hatari enzi hizo wa Brazil Ronaldo Nazario de Lima mwenye mabao 15 ya kombe la dunia. Wachezaji waliofunga mabao mengi kombe la dunia
Mchezaji/Nchi | Mabao |
Ronaldo-Brazil | 15 |
Miroslav Klose-Ujerumani | 14 |
Gerd Muller-Ujerumani | 14 |
Just Fontaine-Ufaransa | 13 |
Pele-Brazil | 12 |
Sandor Kocsis-Hungary | 11 |
Jurgen Klinsmann-Ujerumani | 11 |
Helmut Rahn-Ujerumani | 10 |
Gary Lineker-uingereza | 10 |
Gabriel Batistuta-Argentina | 10 |
"Iwapo Miroslav atacheza katika kikosi cha kwanza au akitokea benchi kwetu ni mchezaji muhimu sana,mchezaji wa kuigwa ndani na nje ya uwanja." alisema Loew
Wenye mabao mengi kombe la dunia
Klose anaweza kuanzia benchi huku Thomas Mueller akipewa nafasi kubwa
Klose alivunja rekodi ya baba yake na Thomas Muller yaani Gerd Mueller ya kuwa mfungaji bora wa Ujerumani kwa miaka 40 baada ya kufikisha mabao 69 wakati Armenia ikifungwa mabao 6-1 na Ujerumani mchezo wa kirafiki.
Mchezo wa leo utaanza saa moja kamili usiku wa leo.
Akiwa amecheza michezo 19 ya kombe la dunias, Klose anaweza kufikia rekodi ya Lothar Matthaeus aliyecheza mechi 25 lakini itategemea na mwenendo wa Ujerumani katika mashindano ya mwaka huu labda ifike hatua ya Nusu au fainali.
0 comments:
Post a Comment