Victoria University mabingwa wa CECAFA Nile Basin
Klabu ya Victoria University ndio Mabingwa wa Mashindano mapya ya CECAFA NILE BASIN baada kuichapa AFC Leopards ya Kenya mabao 2-1 katika Fainali iliyochezwa huko Khartoum International Stadium Jijini Khartoum Nchini Sudan hapo Jana.
Haya ni Mashindano ya kwanza kabisa ya
Kombe hilo yaliyoshindaniwa na Klabu kadhaa kutoka Nchi za Afrika
Mashariki na ya Kati ambao ni Wanachama wa CECAFA.
Kwa ushindi huo, Victoria University pia
wamejinyakulia Donge nono la Dola 30,000 na ni baraka kwa Klabu changa
iliyoshiriki michuano ya CECAFA kwa mara ya kwanza kabisa.
Victoria University ndio waliowatoa
Wawakilishi wa Tanzania Bara, Mbeya City, kwenye Robo Fainali baada ya
kuwafunga Bao 1-0 kwa Bao la Penati.
Kwa kuwa Washindi wa Pili, AFC Leopards walipewa Dola 20,000.
0 comments:
Post a Comment