Baada ya kubeba ubingwa Conte asifiwa na Juve
Juventus walimsifu sana kocha wao Antonio Conte kwa kushinda taji la tatu la Serie
A, baada ya kufufua klabu hiyo kufuatia kashfa ya kupanga mechi, kushushwa
ngazi hadi ligi ya daraja la pili na kukosa kufuzu kwa michuano ya Ulaya.
Kocha huyo mwenye miaka 44, ambaye majuzi alijibizana vikali na
kocha wa zamani wa Juve Fabio Capello, meneja wa Italia Cesare Prandelli, Rudi
Garcia wa Roma na Rafael Benitez wa Napoli, ameifufua Juventus ambayo
hujulikana kwa utani kama Bibi kizee, tangu atue huko 2011.
"Conte aliingiza imani yake
kwenye kikosi siku yake ya kwanza huko, shukrani zake nyingi zinafaa kumwendea
kwani ni tukio la kihistoria,” alisema mkurugenzi Giuseppe Marotta akizungumza na Sky Sport .
Juventus walitwaa taji Jumapili bila
hata kucheza mchezo baada ya AS Roma,
timu pekee ambayo ilikuwa na nafasi ya kushindana nao, kushindwa 4-1 dhidi ya Catania.
Kabla ya Conte kutua huko, Juventus
walikuwa bado wanahangaika baada ya kashfa ya upangaji mechi ambayo ilipelekea
wao kupokonywa mataji ya 2005 na 2006 na kushushwa ngazi hadi Serie B.
Walikuwa wamemaliza ligi ya nyumbani
wakiwa nambari saba kwa misimu miwili mfululizo kabla ya kuteuliwa kwake na
hawakucheza michezo ya Ulaya msimu wake wa kwanza akiwa kwenye usukani, lakini
sasa wanasherehekea kushinda taji lao la 30 baada ya kushinda mara tatu
mfululizo.
Kipa Gianluigi Buffon alisema wakati
muhimu kwao katika kampeni yao ya kuwania ubingwa ulikuwa ushindi wao wa 1-0 dhidi
ya Genoa mwezi Machi baada ya mpira wa adhabu wa Andrea Pirlo kuwakabidhi ushindi kukiwa na
dakika mbili zilizokuwa zimesalia za mchezo huo.
0 comments:
Post a Comment