Wednesday, 10 September 2014

Mwenyekiti wa Ferari astaafu baada ya miaka 23.

Mwenyekiti wa Ferrari  Luca Di Montezemolo amestaafu kuongoza kampuni hiyo inayojihusisha na langalanga baada ya kuongoza kwa miaka 23.

Taarifa zilizonaswa na Sports4lifetz ni  kwamba mwenyekiti huyo amejiuzulu baada ya kuwa na  msimu mbaya.

Di Montezemolo, 67 amesema kuwa baada ya utumishi huo kwa sasa ameamua kuondoka madarakani na anajivunia mafanikio aliyoyapata kwa muda huo.

Sergio Marchionne ndiye atakayechukua mikoba ya  Di Montezemolo, ambaye ataanza kazi Octoba 13

Kampuni ya Ferrari  haijashinda taji lolote kuanzia mwaka  2008

Katika mashindano yaliyomalizika juzi ya  Italia Grand Prix waendesha magari wa Ferari walishika nafasi isiyoridhisha ambapo  Fernando Alonso alitangaza kustaafu huku mwenzake   Kimi Raikkonen akishika nafasi ya 9.
.

0 comments:

Post a Comment