Thursday, 12 June 2014

Breaking news:Fabregas asaini miaka mitano Chelsea

Klabu ya Chelsea  ya Uingereza  imekamilisha usajili wa kiungo wa Barcelona  na mchezaji wa zamani wa Arsenal  Cesc Fabregas.

Klabu hiyo inayoongozwa na Jose Mourinho imetoa kiasi  cha £30 mil kwa ajili ya nyota huyo wa Hispania  ambaye amesaini mkataba wa miaka mitano ndani ya Stamford Bridge.

Fabregas amefunga mabao 8 kwenye  La Liga kwa upande wa  Barcelona kutengeneza mabao   19 katika msimu huu kwa kucheza michezo 36  na kuushukuru uongozi wa klabu hiyo .

Fabregas mwenye miaka 27 amesema kuwa anawashukuru watu wote ndani ya klabu ya Barcelona baada ya kuitumikia kwa miaka mitatu na kusisitiza kuwa ni klabu yake aliyoichezea tokea utotoni.

"Nilikuwa nahisi kuwa sijamaliza kucheza ligi kuu ya Uingereza,na sasa huu ni muda wa kurudi pale.alisema Fabregas

Fabregas alichezea Arsenal kwa miaka nane kabla ya kurudi tena  Barcelona.

0 comments:

Post a Comment