Hispania,Cameroon na Australia kwaherini kombe la dunia
Mabingwa wa Dunia Hispania Jana huko Estadio do Maracanã Jijini Rio de Janeiro Nchini Brazil walinyukwa mabao 2-0 na Chile na kuvuliwa Ubingwa wa Dunia na kutupwa nje ya Fainali za Kombe la Dunia huku wakiwa wamebakisha Mechi moja ya Kundi B dhidi ya Australia ambao nao wametupwa nje.
Hispania, ambao walitandikwa mabao
5-1 Uholanzia kwenye Mechi ya Kwanza ya Kundi B, Jana walifungwa mabao
yote mawili katika Kipindi cha Kwanza mabao yalifungwa na Eduardo Vargas
na
Charles Aranguiz.
Hispania wamekuwa Mabingwa wa kwanza wa
Dunia kutupwa nje kwenye kabla kutinga Raundi ya Kwanza ya Mtoano ya
Fainali za Kombe la Dunia.
Matokeo mengine huko Arena Amazonia Jijini
Manaus Nchini Brazil, Croatia imewafunga Cameroon mabao 4-0 kwenye Mechi ya
Kundi A la Fainali za Kombe la Dunia na kuitupa nje ya Mashindano haya.
Cameroon, wakiwa wamebakisha Mechi moja
ya Kundi A dhidi ya Wenyeji Brazil, wanaungana na Hispania na Australia kuyaaga Mashindao haya.
Lakini Uholanzi imechungulia Raundi
ya Pili baada ya kuichapa Australia mabao 3-2
kwenye Mechi ya Kundi B iliyochezwa Estadio Beira-Rio Mjini Porto
Alegre Nchini Brazil.
Uholanzi walitangulia kwa Bao la
Arjen Robben ambalo lilidumu Dakika 1 tu na Tim Cahill kusawazisha na
kisha Australia kwenda mbele mabao 2-1 Kipindi cha Pili kwa Penati ya Mile
Jedinak.
Lakini Uholanzi walisawazisha Dakika 4
baadae kupitia Nahodha wao Robin van Persie na kupata ushindi kwa Bao
la Memphis Depay.
Huu ni ushindi wa pili mfululizo kwa Uholanzi na kipigo cha pili mfululizo kwa Australia ambao
walichapwa 3-1 na Chile kwenye Mechi ya Kwanza.
Mechi za leo
ALHAMISI, JUNI 19, 2014 |
|||
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
1900 |
Colombia v Ivory Coast |
C |
Nacional |
2200 |
Uruguay v Uingereza |
D |
Arena Corinthians |
0100 |
Japan v Ugiriki |
C |
Estadio das Dunas |
0 comments:
Post a Comment