Ivorycoast waanza vema kombe la dunia.
Mabao mawili ya vichwa katika kipindi cha pili ya Wilfried Bony na Gervinho yameipa ushindi Ivory Coast au Cote d'Ivoire kutoka nyuma na kushinda mabao 2-1 dhidi ya Japan muda mfupi uliopita mechi ya kundi la Group C uwanja wa Pernambuco huko Recife,Brazil.Keisuke Honda aliwapa uongozi vijana wa Alberto Zaccheroni baada ya kufunga bao zuri akikokota mpira kwenye boksi kabla ya kufunga..
Vijana wa Sabri Lamouchi ambaye ni kocha mdogo kuliko wote katika mashindano ya mwaka huu walipwaya kipindi cha kwanza kabla ya kuigia kwa Didier Drogba katika kipindi cha pili.
Ivory coast inakuwa timu ya kwanza kushinda kutoka Afrika baada ya Cameroon kupoteza mchezo wa kwanza dhidi ya Mexico.
Ratiba ya leo.muda kwa saa za Tanzania
JUMAPILI, JUNI 15, 2014 |
|||
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
1900 |
Switzerland v Ecuador |
E |
Nacional |
2200 |
France v Honduras |
E |
Estadio Beira-Rio |
0100 |
Argentina v Bosnia-Herzegovina |
F |
Estadio do Maracanã |
0 comments:
Post a Comment