Kesho ndugu wawili Boateng kupambana tena kombe la dunia
Wakati leo hii Italia ikijiandaa kupepetana na Costarica , Kevin-Prince Boateng na Jerome Boateng ambao ni ndugu kesho (Jumamosi ) watakutana uso kwa uso kwenye Mechi ya Kundi G la Fainali za Kombe la Dunia huko Estadio Castelão Mjini Fortaleza, Brazil.
Siku hiyo, Ghana itaivaa Ujerumani kwenye
Mechi zao za Pili za Kundi G huku Ghana wakiwania ushindi baada ya
kufungwa Mechi yao ya kwanza na Marekani mabao 2-1 na Ujerumani ikitaka
kuendeleza ushindi baada ya kuichapa Ureno mabao 4-0.
Kevin-Prince Boateng, anaechezea Ghana,
ameeleza pambano hilo litakuwa la ‘kufa na kupona’ wakati
atakapokabiliana na Ndugu yake Jerome Boateng anaechezea Ujerumani.
Mwaka 2010, huko Afrika
Kusini, kwenye Fainali za Kombe la Dunia, Kevin-Prince na Jerome,
walivaana wakati Nchi zao zilipokutana na kuweka Historia ya kuwa Ndugu
wa kwanza kabisa kuchezea Timu pinzani.
JUMAMOSI, JUNI 21, 2014 |
|||
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
1900 |
Argentina v Iran |
F |
Estadio Mineirão |
2200 |
Germany v Ghana |
G |
Estadio Castelão |
0100 |
Nigeria v Bosnia-Herzegovina |
F |
Arena Pantanal |
0 comments:
Post a Comment