Friday, 20 June 2014

Sijiuzulu-Hodgson

Kocha wa Uingereza Roy Hodgson amesema hana nia ya kujiuzulu licha ya Timu yake kuchungulia kutupwa nje baada ya kufungwa Mechi yao ya Pili ya Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil.
Jana, mabao mawili ya Luis Suarez, anayecheza Liverpool, yaliwaua Uingereza mabao 2-1 katika Mechi yao ya Pili ya Kundi D.
Kwenye Mechi ya Kwanza Uingereza walipigwa 2-1 na Italy.
Wayne Rooney ndiye aliefunga Bao la England na kufunga midomo ya Watu waliokuwa wakimpinga na sasa hao hao wakingojewa kusema kama watamnanga Steven Gerrard ambaye ndiye alitoa upenyo kwa mwenzake wa Liverpool Suarez kufunga Bao la ushindi.
Ikiwa Leo Italy na Costa Rica zitatoka Sare basi Uingereza wako nje lakini matokeo mengine yanawapa nafasi Uingereza ikiwa wataifunga Costa Rica kwenye Mechi ya mwisho na Matokeo mengine kwenda kwao.
Lakini kocha wa England, Roy Hodgson, amekata kujiuzulu na kuiacha FA iamue inachotaka.

0 comments:

Post a Comment