Sunday, 8 June 2014

Klabu bingwa Afrika TP Mazembe na Zamalek leo jumapili,Etoile yashinda kwa taabu

Klabu ya  Etoile du Sahel jumamosi hii ilitoka nyuma na kushinda mabao   4-3 dhidi ya Nkana ya Zambia katika mashindano ya kombe la Shirikisho barani  Afrika mwaka  2014 na kupanda kileleni mwa kundi la  B.
Mabingwa hao wa mwaka 2006 wamefikisha alama 5 moja zaidi ya  Al Ahly.
Matokeo mengine hiyo jana ni kwamba Asec Mimosas kutoka Ivorycoast ilikibali kichapo cha mabao 3-2 dhidi ya Coton Sport ya Cameroon.
Sewe Sports itacheza leo jumapili na AL Ahly kutoka Misri na AS Real de Bamako itacheza na  AC Leopards de Dolisie
Kwa upande wa klabu Bingwa yaani CAF CHAMPIONZ LIGI TP Mazembe, yenye Wachezaji mahiri wa Tanzania, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu, itakuwa Nyumbani Lubumbashi kuwavaa Wakongwe wa Misri Al Zamalek.
Jumapili Juni 8
TP Mazembe v Al Zamalek
Espérance Sportive de Tunis v Club Sportif Sfaxien

0 comments:

Post a Comment