Pigo kwa Nigeria Echiejile kukosa kombe la dunia 2014
Mchezaji huyo mwenye miaka 26 anayechezea klabu ya Monaco aliumizwa katika suluhu ya 0-0 Nigeria ikicheza na Ugiriki katika mchezo wa kujipima nguvu.
Echiejile baada ya kufanyiwa uchunguzi amebainika kuwa atakaa nje ya dimba kwa wiki 3
Nafasi yake itachukuliwa na winga wa Enugu Rangers anayeitwa Ejike Uzoenyi.
Kocha Stephen Keshi alisema: "dakatari amsema Echiejile anahitaji wiki tatau ili apone,hatuna muda wa kusubiri ili apone,tumeamua kumchukua mchezaji mwingine ."
Nigeria itapambana na Iran, Bosnia-Herzegovina na Argentina katika kundi la F, wataanza na Iran katika uwanja wa Curitiba Juni 16 .
Kikosi cha Nigeria:
Makipa: Vincent Enyeama (Lille), Austin Ejide (Hapoel Be'er Sheva), Chigozie Agbim (Gombe United).
Walinzi: Efe Ambrose (Celtic), Godfrey Oboabona (Rizespor), Azubuike Egwuekwe (Warri Wolves), Kenneth Omeruo (Middlesbrough), Juwon Oshaniwa (Ashdod), Joseph Yobo (Norwich, mkopo kutoka Fenerbahce), Kunle Odunlami (Sunshine Stars).
Viungo: John Mikel Obi (Chelsea), Ramon Azeez (Almeria), Ogenyi Onazi (Lazio), Reuben Gabriel (Waasland-Beveren), Michael Babatunde (Volyn Lutsk), Ejike Uzoenyi (Enugu Rangers).
Washambuliaji: Ahmed Musa (CSKA Moscow), Shola Ameobi (Newcastle), Emmanuel Emenike (Fenerbahce), Michael Uchebo (Cercle Brugge), Peter Odemwingie (Stoke), Victor Moses (Liverpool, on loan from Chelsea), Uche Nwofor (Heerenveen).

0 comments:
Post a Comment