Wednesday, 25 June 2014

Tchakala kocha mpya Togo

Waziri wa michezo nchini Togo  amethibitisha rasmi uteuzi wa Tchanilé Tchakala kuwa kocha mpya wa timu hiyo baada ya mkataba wa aliyekuwa kocha wa Togo mfaransa Didier Six kutoongezwa mwezi januari..
Tchakala alikuwa msaidizi wa  Six  na pia aliwahi kuwa katika benchi la ufundi mwaka  2013 katika mashindno ya AFCON .

Tchakala ni kaka wa Tchanilé Bana, ambaye aliifundisha  Togo kati ya mwaka  2000 na  2002   ambaye alituhumiwa kuiongoza Togo kucheza mchezo wa kirafiki dhidi ya  Bahrain  September 2010. Kocha huyo ataanza kibarua cha kuiongoza Togo kufuzu mashindano ya mataifa ya Afrika kule nchini Morocco.
Amepewa mkataba wa miezi sita na utaongezwa iwapo ataonsha kazi nzuri,kwa mujibu wa waziri wa michezo.

0 comments:

Post a Comment