Uingereza nje,pata ratiba ya leo kombe la dunia
Bao la Dakika ya 44 Bryan Ruiz,
anaechezea Fulham, limewapa ushindi wa Bao 1-0 Costa Rica walipocheza na
Italia huko Arena Pernambuco, Jijini Fortaleza Nchini Brazil kwenye
Mechi ya Kundi D la Fainali za Kombe la Dunia.
Mbali ya Costa Rica kushinda, Matokeo hayo sasa yamethibitisha rasmi Uingereza wako nje ya Fainali hizi na sasa watakamilisha Ratiba tu kwa
kucheza na Costa Rica Mechi ya mwisho hapo Jumanne Juni 24.
Hii itakuwa mara ya kwanza kwa Uingereza kutolewa hatua za makundi baada ya miaka 56 iliyopita.
Matokeo mengine jana Ufaransa imejiweka nafasi nzuri mno ya kutinga Raundi ya Pili ya Mtoano ya Fainali za Kombe la
Dunia baada kuitandika Switzerland mabao 5-2 katika Mechi yao ya Kundi E
iliyochezwa huko Arena Fonte Nova huko Jijini Salvador.
Katika Mechi nyingine ya Kundi E hiyo Jana, Ecuador iliwafunga Honduras mabao 2-1 na kujikita nafasi ya Pili nyuma ya Ufaransa.
Hii leo Kevin-Prince Boateng na Jerome
Boateng ambao ni ndugu watakutana uso kwa uso kwenye Mechi ya Kundi G la
Fainali za Kombe la Dunia huko Estadio Castelão Mjini Fortaleza, Brazil.
Siku hiyo, Ghana itaivaa Ujerumani kwenye
Mechi zao za Pili za Kundi G huku Ghana wakiwania ushindi baada ya
kufungwa Mechi yao ya kwanza na Marekani mabao 2-1 na Ujerumani ikitaka
kuendeleza ushindi baada ya kuichapa Ureno mabao 4-0.
Kevin-Prince Boateng, anaechezea Ghana,
ameeleza pambano hilo litakuwa la ‘kufa na kupona’ wakati
atakapokabiliana na Ndugu yake Jerome Boateng anaechezea Ujerumani.
Mwaka 2010, huko Afrika
Kusini, kwenye Fainali za Kombe la Dunia, Kevin-Prince na Jerome,
walivaana wakati Nchi zao zilipokutana na kuweka Historia ya kuwa Ndugu
wa kwanza kabisa kuchezea Timu pinzani.
| JUMAMOSI, JUNI 21, 2014 |
|||
|
SAA |
MECHI |
KUNDI |
UWANJA |
|
1900 |
Argentina v Iran |
F |
Estadio Mineirão |
|
2200 |
Germany v Ghana |
G |
Estadio Castelão |
|
0100 |
Nigeria v Bosnia-Herzegovina |
F |
Arena Pantanal |

0 comments:
Post a Comment