Sunday, 6 July 2014

Apumzike kwa amani,Toure azikwa Ijumaa

Ibrahim Toure,enzi za uhai wake
Ibrahim Oyala Toure ambaye ni mdogo wa wachezaji ndugu wa  Ivory Coast Yaya na Kolo Toure,aliyefariki jijini  Manchester  June 19, amezikwa mjini Abidjan siku ya  ijumaa wakiwemo kaka zake na watu wengine.
Mamia ya mashabiki  walivaa mavazi meupe  ili kutoa heshima zao za mwisho kwa mshambuliaji  huyo mwenye miaka  29.
Familia ya Toure
Waziri wa michezo wa Ivory Coast Alain Lobognon aliiwakilisha serikali katika msiba huo.
Toure hakuwa maarufu sana kutokana na kutoitwa timu ya taifa lakini msiba wake ulishtua watu wengi baada ya kaka zake kuwepo kwenye mashindano ya kombe la dunia 2014 Brazil wakiiwakilisaha Ivory Coast.
Kama ilivyo kwa kaka yake,Toure alianza soka katika akademi ya  Asec Mimosas ya mjini  Abidjan. Aliwahi kuicheza  Lebanese ya Al Safa, Metallurg Donestk nchini Ukraine, klabu ya  Nice ya Ufarana na  Misr El Maqasa ya Misri.

0 comments:

Post a Comment