Uholanzi yatinga nusu fainali kucheza na Argentina,Angel Di Maria nje kombe la dunia.
Timu ya taifa ya Uholanzi imeingia hatua ya nusu fainali baada ya kushinda kwa mikwaju ya pelnati 4-3 dhidi ya Costa Rica,baada ya dakika 120 matokeo ikiwa ni suluhu.Golkipa wa Newcastle Tim Krul aliingizwa dakika za mwisho kabla ya filimbi ya mwisho na kocha wake Louis van Gaal - mabadiliko yaliyoonesha matokeo mazuri kwa Uholanzi.
Costa Rica iliwadhibiti sana Uholanzi katika nafasi ya Ulinzi huku kipa Keylor Navas aking'ara golini.
Wesley Sneijder alikosasakosa mabao baada ya shuti zake mbili kugonga mwamba wa pembeni na wa juu.
Kipa aliyetoka benchi Tim Krul, aliokoa pelnati ya nahodha wa Costarica Bryan Ruiz na pelnati ya Michael Umana na timu kushinda 4-3.
Wakati hayo yakiendelea mchezaji wa Argentina Angel Di Maria atakosa mechi za kombe la dunia kwa timu yake baada ya kuumia msuli wa nyama ya pajani wakati Argentina ikiibamiza Ubelgiji bao 1-0 katika mchezo wa kwanza mapema leo.
Brazil itapambana na Ujerumani mechi ya nusu fainali huku Neymar akikosekana ilhali Uholanzi itacheza na Argentina.
NUSU FAINALI JUMANNE, JULAI 8, 2014 |
|||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
2300 | Ujerumani v Brazil [61] | NUSU FAINALI | Estadio Mineirão, Belo Horizonte | ||||||
JUMATANO, JULAI 9, 2014 | |||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
2300 | Argentina v Uholanzi [62] | NUSU FAINALI | Arena Corinthians, Sao Paulo | ||||||
MSHINDI WA TATU JUMAMOSI, JULAI 12, 2014 |
|||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
2300 | Aliyefungwa 61 v Aliyefungwa 62 | MSHINDI WA 3 | Nacional, Brasilia | ||||||
FAINALI JUMAPILI, JULAI 13, 2014 |
|||||||||
SAA | MECHI | KUNDI | UWANJA | ||||||
2200 | Mshindi Mechi 61 v Mshindi Mechi 62 | FAINALI | Estadio do Maracanã, Rio de Janeiro |
0 comments:
Post a Comment