Bora Suarez aliyeng'ata kuliko Matuidi aliyefanya faulu mbaya-Maradona.
Maradona amesema kuwa mfaransa huyo alimfanyia makosa makubwa sana Onazi na ni hatari kuliko ya Luis Suarez aliyemng'ata meno mlinzi wa Italia Giorgio Chiellini.
"Haiwezekani mwamuzi kutokuchukulia tukio lile kama uhalifu. Ilikuwa mbaya sana kuliko aliyoyafanya Suarez dhidi ya Chiellini," alisema Maradona
Matuidi alitenda tukio hilo ambapo Ufaransa ilishinda mabao 2-0 na baada ya mchezo kumalizika alikwenda kuomba msamaha ndani ya chumba cha kubadilishia nguo cha Nigeria.
1 comments:
Maradona kasema ukweli,Msamaha wa nini wakati aliishatuumiza na ndichio chanzo cha kuidhoofisha timu yetu???Nawashangaa FIFA kwa nini wanakataa kutumia ushahidi wa video kutoa haki wakati wanaweza kumuadhibu mtu kwa kutumia ushahidi wa video???Wapuuzi sana
3 July 2014 at 14:32Post a Comment