Monday, 7 July 2014

Brazil na Ujerumani kuchezeshwa na mwamuzi aliyechezesha Uruguay na Italia

Shirikisho la soka dunianai FIFA imetangaza mwamuzi wa Mechi ya Nusu Fainali ya Kombe la Dunia kati ya Brazil na Ujerumani.
Mwamuzi huyo ni yule aliyechezesha mchezo ambao sasa umeshika vichwa vya watu wengi Duniani  kati ya Italia na Uruguay  katika kombe la Dunia huko Brazil ambapo mchezaji wa Uruguay, Luis Suarez, alimng’ata Meno Beki wa Italia Giorgio Chiellini bila mwaamuzi huyo kuona tukio hilo na kutochukua hatua yeyote hata baada ya Chiellini kumkimbilia na kuvua Jezi kuonyesha alama za Meno.
Mwamuzi huyo kutoka Mexico ni Marco Rodríguez, mwenye Miaka 40 atasimama katikati ya uwanja hiyo kesho

Hii ni mara ya 3 kwa mwamuzi huyo kuchezesha Fainali za Kombe la Dunia,Mbali ya Mechi  ya Uruguay na Italy,  pia amechezesha Mechi nyingine huko Brazil ni ile ya Ubelgiji v. Algeria.

0 comments:

Post a Comment