David Luiz aomba msamaha baada ya kipigo cha 7-1
Beki na nahodha msaidizi wa timu ya taifa ya Brazil, David Luiz , ameomba radhi mashabiki wa soka wa nchi hiyo kufuatia kipigo cha mabao 7-1 walichokipokea kutoka kwa Ujerumani jana usiku mjini Belo Horizonte.Ndoto za Brazil kubeba kombe kama wenyeji zilitoweka baada ya Ujerumani kuongoza mabao 5-0 katika kipindi cha kwanza.
Shabiki akitokwa na machozi |
Amesema wanatambua mashabiki wa soka nchini humo, wameumizwa na kichapo hicho, lakini akasisitiza hawana budi kusamehewa na kuendeleza umoja waliokuwa nao kama walivyoanza fainali za kombe la dunia za mwaka huu June 12.
''Katika maisha yangu,nimejifunza kuwa m
![]() |
Mashabiki hawaamini kinachoendelea Brazil v Ujerumani |
Kwa upande wa mlinda mlango wa Brazil, Julio Cesar amesema soka lina maajabu yake na usiku wa kuamkia hii leo, maajabu ya hatari yaliwageukia wao kama wenyeji, hivyo hawana budi kukubaliana na hili hiyo.
Timu ya taifa ya Brazil imekubali kufungwa mabao 7-1 na kuwa timu ya kwanza duniani kufungwa idadi hiyo ya mabao katika mchezo wa hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la dunia.
0 comments:
Post a Comment