Monday, 21 July 2014

Matokeo Kuelekea AFCON 2015,timu zilizoanzia nyumbani mambo safi,isipokuwa Tanzania.

Benin, Lesotho na Congo Brazzaville zimeshinda mechi zao za awali kufuzu AFCON mwaka 2015 Nchini Morocco
Bao pekee la Benin limefungwa na mchezaji wa klabu ya  West Bromwich Albion,Stephane Sessegnon . Alifunga bao pekee dakika ya  19 na kuwalaza Malawi 1-0 mjini Cotonou.
Mchezo ulimalizkia kwa timu zote kuwa pungufu baada ya Wachezaji   Badarou Nafiou wam Benin na Mmalawi  Frank Banda kulimwa kadi nyekundu katika dakika ya 84.
Timu zote zilizoanzia nyumbani zilishinda isipokuwa Tanzania ambao wametoka sare ya 2-2 na Msumbiji.

  • Jumamosi
  • Botswana 2-0 Guinea-Bissau
  • Uganda 2-0 Mauritania
  • Sierra Leone 2-0 Seychelles
  • Jumapili
  • Lesotho 1-0 Kenya
  • Tanzania 2-2 Msumbiji
  • Congo Brazzaville 2-0 Rwanda
  • Benin 1-0 Malawi
Lesotho ilishinda bao 1-0 dhidi ya  Kenya mjini Maseru.
Rwanda, ambayo iliitoa Libya katika raundi iliyopita , ilibamizwa mabao 2-0 na Congo-Brazzaville mjini Pointe-Noire.
Mabao ya Congo yalifungwa na Cesaire Gandze pamoja na  Ferebory Dore.
Michezo ya marudiano itapigwa kati ya Agosti1-3. Michezo ya AFCON 2015 Morocco itachezwa kuanzia Januari 17 hadi  Februar 8 2015.

0 comments:

Post a Comment