Monday, 21 July 2014

Pigo Manchester City,Negredo avunjika guu la upande wa kulia

Klabu ya Manchester City imepata pigo baada ya Mshambuliaji wake Alvaro Negredo kuthibitika kuwa amevunjika mguu wake utakaomfanya kukaa nje ya uwanja kwa miezi kadhaa. 
Negredo mwenye umri wa miaka 28 aliumia katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Hearts jana na kuthibitisha taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Instagram sambamba na picha ya mguu wake wa kulia ukiwa na bandeji gumu. 
Nyota huyo aliandika kuwa anawajulisha mashabiki wake kuwa miezi michache inayokuja itakuwa migumu kwake kutokana na kuvunjika mguu. 
Hata hivyo aliwaondoa hofu mashabiki hao kwa kuwaambia kuwa atarudi akiwa imara zaidi zaidi ya alivyo sasa. 
Taarifa zitakuwa ni mbaya kwa kocha Manuel Pellegrini wakati City wakitaka kutetea taji lao la ligi walilonyakuwa msimu uliopita.

0 comments:

Post a Comment