Saturday, 12 July 2014

Wanaowania tuzo za kombe la dunia 2014 Kwenye picha tofauti.

Shirikisho la soka duniani FIFA imetangaza Majina ya Wachezaji 10 watakaogombea Tuzo ya Mchezaji Bora wa Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil, Tuzo ya Mpira wa Dhahabu.
Listi hiyo ya Wachezaji 10 inao Wachezaji Wanne kutoka Ujerumani, Watatu wa Argentina huku Colombia, Brazil na Uholanzi  zikitoa Mchezaji mmpja moja.
Wachezaji wa Argentina ambao wako kwenye Lisi hiyo ni Angel Di Maria, Javier Mascherano na Lionel Messi.
Ujerumani ni Mats Hummels, Toni Kroos, Phillip Lahm na Thomas Muller.
Waliobaki ni Straika wa Colombia James Rodriguez, Nyota wa Brazil Neymar na Arjen Robben wa Uholanzi.
‘GLOVU YA DHAHABU’
Vile vile FIFA imateja Majina ya Makipa Watatu ambao watawania Tuzo ya Kipa Bora wa Fainali za Kombe la Dunia za Mwaka 2014 huko Brazil.
Manuel Neur
Kipa Bora atapewa Tuzo ya Glovu ya Dhahabu.
Makipa hao ni Kipa wa Costa Rica Keylor Navas, Manuel Neuer wa Germany na Kipa wa Argentina Sergio Romero.
‘MCHEZAJI BORA KIJANA’
Pia, mshambuliaji wa Uholanzi Memphis Depay pamoja na Paul Pogba na Raphael Varane wa Ufaransa wameteuliwa kugombea Tuzo ya Mchezaji Bora Kijana.
Depay Memphis
Washindi wote wa Tuzo hizo watatangazwa mara baada ya Fainali ya Jumapili kati ya Argentina na Ujerumani  huko Estadio Maracana, Rio de Janeiro.
Angel Di Maria scores late winner for Argentina
Angel Di Maria  akishangilia bao la ushindi Argentina ikishinda kwa Uswisi

Argentina's Lionel Messi
Lionel Messi akishangilia bao lake dhidi ya Iran
World Cup 2014: Arjen Robben puts Netherlands ahead
Arjen Robben  akishangilia ushindi wa 5-1 dhidi ya Hispania

Highlights: Netherlands 0-0 Argentina (2-4 pens)
Argentina wakishangilia

Brazil striker Neymar celebrates scoring Brazil's second goal
Neymar akishangilia bao dhidi ya Croatia

World Cup 2014: Colombia's James Rodriguez
James Rodriguez AMEFUNGA MABAO 6

Germany's Thomas Mueller celebrates his third goal against Portugal
Thomas Muller alifunga  hat-trick dhidi ya  Portugal

Germany's Thomas Muller and Andre Schurrle celebrate against Brazil
Ujerumani iliposhinda  7-1 dhidi ya Brazil

Toni Kroos scores Gemany's third goal
Toni Kroos akishangilia bao  la tatu dhidi ya  Brazil

Mats Hummels heads Germany in front against France
Mats Hummels akishangilia bao dhidi ya Ufaransa


Mexico's Guillermo Ochoa
Ochoa naye alijitahidi lakini hayupo kwenye list

0 comments:

Post a Comment