Saturday, 23 August 2014

Kikosi cha Cameroon chatangazwa,Nahodha Eto'o aachwa tena.

Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Cameroon Volker Finke ametangaza kikosi chake kwa ajili ya kufuzu AFCON 2015 michezo dhidi ya  DR Congo hapo  September 6 na Ivory Coast  September 10 bila ya nahodha wake  Samuel Eto’o.
Wachezaji wengine waliotemwa ni Aurelien Chedjou, Benoit Assou-Ekotto, Jean II Makoun, Achille Webo na  Charles Itandje wakati mchezaji wa  Barcelona Alexandre Song anatumikia adhabu ya michezo mitatu baada ya kufanya makosa kombe la dunia  2014 kule nchini Brazil.
Finke amewaita wachezaji  25, ambao wataanza kuingia kambini  September 1 mjini Yaounde.

Cameroon imepangwa kundi C sambamba na  Ivory Coast, DR Congo na Sierra Leone.
KIKOSI KAMILI
Makipa: Guy-Rolland Ndy Assembe (Guingamp, France), Pierre-Sylvain Abogo (Tonnerre de Yaounde), Fabrice Ondoua (FC Barcelona, Spain). Walinzi : Cedric Djeugoue (Coton Sport), Nicolas Nkoulou (Marseille, France), Joel Matip (Schalke 04, Germany), Gaetan Bong (Olympiakos, Greece), Frank Bagnack (FC Barcelona, Spain), Jerome Guihota (Valenciennes, France), Ambroise Oyongo Bitolo (New York Red Bulls, USA)
Viungo : Eyong Enoh (Antalyaspor, Turkey), Stephane Mbia (FC Seville, Spain), Landry Nguemo (sans club), Raoul Loé (Osasuna, Spain), Edgar Salli (Monaco, France), Georges Mandjeck (Kayseri Erciyesspor, Turkey), Guy-Christian Zock (Cosmos Bafia), Marc Kibong Mbamba (Konyaspor, Turkey)
Washambuliaji: Eric-Maxim Choupo Moting (Schalke 04, Germany), Benjamin Moukandjo (Nancy, France), Vincent Aboubakar (Lorient, France), Jean-Marie Dongou (FC Barcelona, Spain), Léonard Kweuke (Caykur Rizespor, Turkey), Clinton Njie (Lyon, France), Franck Etoundi (FC Zurich, Switzerland)

0 comments:

Post a Comment