Di Maria kutua Manchester United,Kuvaa jezi namba 7.
Klabu ya Manchester United inakaribia kumnasa winga wa Real Madrid Ángel Fabián Di María Hernández kwa uhamisho ambao utavunja rekodi ndani ya Old traford.
Mchezaji huyo mwenye miaka 26 ni mchezaji ambaye aliwindwa sana na klabu hiyo inayofundishwa na mholanzi Louis Van Gaal.Mtandao wa skysports na goal.com umeeleza kuwa Di Maria atasajiliwa kwa kiasi kati ya 60-70 million sawa na Euros (£48-56m) .Taarifa zinadai kuwa Di Maria amekubali dili hiyo na mazungumzo yanaendelea na atakwenda Old traford wiki ijayo.
Mchezaji huyo wa zamani wa Benfica ni wazi kuwa huduma yake imekwisha ndani ya Madrid baada ya kocha Carlo Ancelotti kusema kuwa Di Maria amegoma kuongeza mkataba Bernabeu.
Ujio wa James Rodriguez na Toni Kroos ndani ya Madrid umehamasisha zaidi Di Maria kujiunga na Manchester United.
Di Maria atavaa jezi namba 7 ndani ya Man U jezi ambazo zimevaliwa na nyota David Beckham, Eric Cantona, Cristiano Ronaldo, George Best na Bryan Robson.
Sports4lifetz inafuatilia taarifa hizi kwa undani zaidi.
Wasifu wake |
---|
Jina kamili | Ángel Fabián Di María Hernández | ||
---|---|---|---|
Kuzaliwa | 14 February 1988 | ||
Sehemu alipozaliwa | Rosario, Argentina | ||
Nafasi uwanjani | Winga / kiungo mshambuliaji | ||
Vilabu | |||
Kwa sasa
|
Real Madrid | ||
Namba | 22 | ||
Vijana | |||
1995–2005 | Rosario Central | ||
wakubwa | |||
Mwaka | Team | Amecheza mara | (mabao) |
2005–2007 | Rosario Central | 35 | (6) |
2007–2010 | Benfica | 76 | (7) |
2010– | Real Madrid | 124 | (22) |
Timu ya taifa | |||
2007 | Argentina U20 | 13 | (3) |
2008 | Argentina U23 | 6 | (2) |
2008– | Argentina | 52 | (10) |
0 comments:
Post a Comment