Baada ya kutimuliwa Esperance,Krol kocha mpya Al-Ahli.
Krol ana uzoefu na soka la bara la Africa baada ya kufundisha soka akiwa Misri,Afrika kusini na Tunisia.
Atajiunga na mabingwa hao mara 11 wa Libya Novemba 1.
Baada ya kupata nafasi hiyo Krol amesema kuwa anajua sana soka la Afrika kwa hiyo kwenda kufundisha soka Libya hakumpi taabu yoyote.
Nyota huyo wa zamani,65 alikuwa kocha wa timu ya taifa ya Tunisia ambapo timu iligaragazwa na Cameroon 4-1 kufuzu kombe la dunia 2014 Brazil.
Krol amesema kuwa hali ya machafuko ya kisiasa nchini Libya si tatizo kwake.
0 comments:
Post a Comment