UEFA kuendelea leo,Drogba hatacheza kisa kuwasubiri Arsenal.
Ligi ya mabingwa barani Ulaya,UEFA hatua ya makundi inaendelea leo katika viwanja mbalimbali.Kuelekea michezo hiyo klabu ya Chelsea imeamua kumbakisha nyota Didier Drogba jijini London wakati klabu hiyo ikisafiri hadi Lisbon, Ureno kucheza na Sporting Lisbon.
Chelsea haikutamka lolote kwanini ameachwa hasa ukizingatia hali ya Diego Costa ambaye anakabiliwa na matatizo ya Msuli wa Pajani kiasi cha kushindwa kufanya Mazoezi kama ilivyoelezwa na Jose Mourinho.
Lakini wadadisi wanadai kuwa Drogba ameachwa ili ajifue vema kwa ajili ya mchezo wa wikiendi hii kati ya Chelsea na Arsenal huku ikidaiwa kuwa Drogba ana rekodi nzuri ya kuwafunga Arsenal.
Mabingwa wa soka nchini Uingereza Manchester City ambao watakuwa wenyeji wa AS Roma ya Italia katika mchezo wa kundi E utakaofanyika katika Uwanja wa Etihad.
City wataingia katika mchezo wakihitaji ushindi baada ya kupoteza mchezo wao kwanza waliochezwa na mabingwa wa Ujerumani Bayern Munich ambao walifungwa bao 1-0 huko Allianz Arena.
RATIBA SEPTEMBA 30
CSKA Moscow | v | FC Bayern München | Arena Khimki | 19:00 | ||
FC Schalke 04 | v | NK Maribor | VELTINS-Arena | 21:45 | ||
Paris Saint Germain | v | Barcelona | Parc des Princes | 21:45 | ||
Shakhtar Donetsk | v | FC Porto | Arena Lviv | 21:45 | ||
Sporting Lisbon | v | Chelsea | Estadio José Alvalade | 21:45 | ||
BATE Borisov | v | Athletic Club | Borisov Arena | 21:45 | ||
Manchester City | v | Roma | Etihad Stadium | 21:45 | ||
APOEL Nicosia | v | Ajax | GSP Stadium | 21:45 |
0 comments:
Post a Comment