Tuesday, 2 September 2014

Rekodi ya usajili Uingereza,Van Gaal aweka rekodi huku EPL ikitumia £835m,ni rekodi mpya.

Baada ya  Radamel Falcao kutua ndani ya klabu ya  Manchester United rekodi imewekwa rasmi katika ligi hiyo ya Uingereza  baada ya kiasi cha £835m kutumika katika msimu huu.

Kwenye Siku ya mwisho, Falcao amehamia Man United kutoka AS Monaco kwa Mkopo kwa Pauni Milioni 6, Daley Blind kutoka Ajax na kutua Man United kwa Pauni Milioni 13.8 na Danny Welbeck kuuzwa na Man United kwa Arsenal kwa Pauni Milioni 16,imewafanya  United washikilie rekodi ya usajili msimu huu.


Lakini mapema wiki hii United iliweka rekodi ya usajili mkubwa nchini Uingereza kwa kumnunua  Angel Di Maria kwa kiasi cha £59.7m.

Wachambuzi wa uchumi wamedai kuwa kocha Louis van Gaal ametumia kiasi cha £150m  na kuwa kocha wa kwanza msimu huu kutumia pesa nyingi katika usajili.

Liverpool imetumia kiasi cha  euro mil 117 na Man city imetumia kiasi cha euro millioni  91.1,angalia jedwali hapo chini.


UHAMISHO WA FEDHA NYINGI KATIKA MSIMU HUU.

Angel Di Maria [Real Madrid - Manchester United] £59.7m
Alexis Sanchez [Barcelona - Arsenal] £35m
Diego Costa [Atletico Madrid - Chelsea] £32m
Eliaquim Mangala [FC Porto - Manchester City] £32m
Cesc Fabregas [Barcelona - Chelsea] £30m
Ander Herrera [Athletic Bilbao - Manchester United] £29m
Romelu Lukaku [Chelsea - Everton] £28m
Luke Shaw [Southampton - Manchester United] £27m (Could rise to £31m)
Adam Lallana [Southampton - Liverpool] £25m
Dejan Lovren [Southampton - Liverpool] £20m
Lazar Markovic [Benfica - Liverpool] £20m




0 comments:

Post a Comment