Tuesday, 9 September 2014

Uingereza yaanza vizuri kufuzu EURO 2016,pata matokeo mengine.

Michezo ya kufuzu EURO 2016 imeendelea tena jana na Katika Mechi ya kwanza ya Kundi E iliyochezwa St Jakob Park Mjini Basel, Wenyeji Uswisi walifungwa mabao 2-0 na Uingereza

Uingereza  walipata Bao lao la kwanza katika Dakika ya 58 kupitia Danny Welbeck baada ya nahodha  Wayne Rooney kuunasa Mpira upande wake wa Uwanja na kupanda juu  kisha kumpa pande safi Raheem Sterling alyempasia  Welbeck na kufunga kwa ugoko.

Bao la Pili la Uingereza  lilifungwa Dakika ya 94 tena na Danny Welbeck baada Rickie Lambert, alieingizwa kuchukua nafasi ya Rooney, kumpasia Sterling ambaye alimsogezea Welbeck na kumalizia.


MATOKEO:

Jumatatu Septemba 8

Russia 4 Liechtenstein 0

Luxembourg 1 Belarus 1

Austria 1 Sweden 1

San Marino 0 Lithuania 2

Spain 5 Macedonia 1

Estonia 1 Slovenia 0

Switzerland 0 England 2
Ukraine 0 Slovakia 1

Montenegro 2 Moldova 0

Mechi za Makundi EURO 2016 zinaendelea Jumanne Usiku.
Jumanne Septemba 9

 Kazakhstan v Latvia

 Azerbaijan v Bulgaria

Croatia v Malta

 Norway v Italy

 Czech Republic v Netherlands

 Iceland v Turkey
Andorra v Wales

 Israel v Belgium

0 comments:

Post a Comment