Thursday, 25 September 2014

Van Gaal aendelea kununua wachezaji wa Argentina,ameandaa £40 kwa ajili ya Otamendi.

Kocha wa Manchester United  Louis Van Gaal  bado anaendelea na harakati za kutengeneza nafasi ya ulinzi baada ya klabu yake kuteseka kulinda mabao baada ya kichapo cha  4-0 na 5-3dhidi ya  MK Dons na Leicester City.

Katika kuepuka aibu hiyo  Van Gaal anajiandaa kumnunua Nicolas Otamendi.

Mlinzi huyo raia wa  Argentina ameaandaliwa kiasi cha  £40 million na Van Gaal.

Mashabiki wa United wanashangaa iweje mholanzi huyo amnunue beki huyo kwa £40 wakati  Valencia ilitoa kiasi cha £9.5 million kwa mlinzi huyo mwezi February kutoka Porto.

Lakini ripoti huko Hispania zinadai kuwa  Valencia  haitamuuza  Otamendi, ingawa  United iko tayari kutoa  £40 million.
Otamendi akifanikiwa kutua Old Traford ataungana na Rojo pamoja na Di Maria wakiwa ni raia wa Argentina.

0 comments:

Post a Comment