Thursday, 25 September 2014

Chelsea iko tayari kumuuza Ramires kwenda Madrid

Kwa mujibu wa ripoti mbalimbali nchini Uingereza, klabu ya Chelsea iko tayari kumuuza mchezaji  Ramires, ambaye anawindwa na mabingwa wa Ulaya klabu ya Real Madrid huku ikiwa na lengo la kumnunua Ross Barkley kutoka Everton.

Madrid inayofundishwa na Carlo Ancelotti  iko tayari kumnunua Ramires.
 
Chelsea maarufu kama the  Blues inaweza ikafanikiwa kumnasa mchezaji huyo ambaye anawindwa na Manchester City lakini  City itabanwa na sheria ya matumizi ya fedha.

Ramires ameanza michezo miwili tu ndani ya utawala wa  Mourinho.

Chelsea inahitaji kiasi cha  £25 million kwa ajili ya Mbrazil huyo na imeandaa  kiasi cha  £30 million kwa ajili ya  Barkley,ambaye mwenyewe amekiri kuitamani Chelsea kuliko  Manchester.

0 comments:

Post a Comment