Ferguson hana lawama hata kidogo-Rio Ferdinand.
![]() |
|
|
|
Beki maarufu wa zamani wa miamba wa Uingereza Manchester United, amemfagilia mwalimu mstaafu Sir Alex Ferguson kutokana na aibu inayokumba na vigogo hao wakati huu.
United waliporomoka sana baada ya kuwika katika mchezo wa
ngazi ya juu Uingereza kwa zaidi ya miongo miwili walipomaliza nafasi ya
saba msimu wa mwaka jana chini ya ya utawala wa David Moyes, ambaye alimrithi Ferguson.
Kocha mpya, Louis Van Gaal, ameshindwa kurudisha hadhi ya klabu hiyo na kuzua hisia kuwa Ferguson aliacha klabu hicho katika hali mbaya zaidi baada ya kukiongoza kushinda taji la Uingereza la msimu wa 2012/13.
Kulingana na Ferdinand ambaye aliondoka United mwishoni mwa msimu uliopita alikanusha vikali tetesi kwamba Moyes alirithi kikosi kibovu kutoka Ferguson.
“Sielewi sababu ya kusema hivyo kwani kulikuwa na wachezaji wakuu walioshinda ligi alama 11 mbele ya waliofuata. Ni lazima uwe timu bora kufikia utukufu huo.
“Basi mambo yalianza kuporomoka lini? Ni sababu ya Ferguson? Watu wanadaiaje hilo? Sifikirii lawama lielekezwe kwa Ferguson na kuondoka kwake baada ya kushinda taji ni jambo bora sana,” Ferdinand ambaye anachezea QPR aliongeza.
Kocha mpya, Louis Van Gaal, ameshindwa kurudisha hadhi ya klabu hiyo na kuzua hisia kuwa Ferguson aliacha klabu hicho katika hali mbaya zaidi baada ya kukiongoza kushinda taji la Uingereza la msimu wa 2012/13.
Kulingana na Ferdinand ambaye aliondoka United mwishoni mwa msimu uliopita alikanusha vikali tetesi kwamba Moyes alirithi kikosi kibovu kutoka Ferguson.
“Sielewi sababu ya kusema hivyo kwani kulikuwa na wachezaji wakuu walioshinda ligi alama 11 mbele ya waliofuata. Ni lazima uwe timu bora kufikia utukufu huo.
“Basi mambo yalianza kuporomoka lini? Ni sababu ya Ferguson? Watu wanadaiaje hilo? Sifikirii lawama lielekezwe kwa Ferguson na kuondoka kwake baada ya kushinda taji ni jambo bora sana,” Ferdinand ambaye anachezea QPR aliongeza.
0 comments:
Post a Comment