Monday, 13 October 2014

Wenger aomba msamaha baada ya kumsukuma Mourinho.

Kocha wa klabu ya  Arsenal,Arsene Wenger ameomba radhi kwa kitendo chake cha kumsukuma kocha wa Chelsea  Jose Mourinho katika mchezo wa ligi kuu ya Uingereza uliopigwa Octoba 5 katika uwanja wa Stamford Bridge.

"Watu wameipa sana kipaumbele tukio hili lakini sijawahi kufanya tukio kama hili katika soka. Ninajutia kwa tukio nililofanya na ninaomba msamaha," Wenger aliimbia runinga ya taifa ya Ufaransa  TF1.

Wenger alikwenda kumsukuma  Mourinho sehemu ya kifua chake katika mchezo huo uliomalizika kwa Chelsea kushinda mabao  2-0  October 5 mwaka huu.

Akizungumza na TF1, Mourinho amesema ''sitazungumzia chochote. Sina la kuongezea katika picha ambazo dunia imeshuhudia''.

0 comments:

Post a Comment