Tuesday, 14 October 2014

Kluivert atemwa kwa wanaowania ukocha Ghana,Shuster aitwa.

Mjerumani Bernd Schuster ameingia kwenye listi ya tano bora ya makocha wanaotafutwa ili mojawapo awe kocha wa Ghana na kumrithi  Patrick Kluivert ambaye jina lake limeondolewa na shirikisho la soka la Ghana  (GFA).

GFA imesema kuwa mholanzi huyo ameondolewa katika mbio hizo na watakaobaki watamrithi Kwesi Appiah.
 
Majina ya makocha yaliyobaki ni kocha wa zamani wa Chelsea  Avram Grant,kiungo wa zamani wa Italy  Marco Tardelli, mswisi Michel Pont na  mhispania  Juan Ignacio Jimenez.


"Pont na  Tardelli watafanyiwa usaili mjini  Accra  October 17, wakati Grant na Jimenez wataenda October 18," imesema  GFA.

Nyota huyo wa zamani wa  Real Madrid , Schuster, ataitwa ili kufanya usaili ndani ya siku hizo.

Schuster ni baadhi ya wachezaji wachache waliong'ara na  Real Madrid na kujiunga na watani wa jadi Barcelona, na kushinda mataji.

Alisaidi Ujerumani kubeba ubingwa wa ulaya mwaka 1980, baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Ubelgiji katika fainali.

0 comments:

Post a Comment