Friday, 7 November 2014

EPL kuendelea tena kesho,Liverpool na Chelsea kupepetana.

Ligi kuu ya kandanda nchini Uingereza itaendelea tena  Jumamosi hii ambapo mechi ya mapema itakuwa katika uwanja wa  Anfield  kati ya Liverpool na Vinara wa Ligi Chelsea.

Mechi hii, itakayoanza Saa 9 Dakika 45 alasiri, inazikutanisha Liverpool, walio Nafasi ya 7 kwenye Ligi, na Vinara wa Ligi Chelsea walio alama  12 mbele yao.

Ikumbukwe kuwa Timu zote hizi mbili zinatoka kwenye Mechi za ligi ya mabingwa barani Ulaya   wakati Liverpool, ilifungwa 1-0 huko Hispania na Mabingwa wa Ulaya Real Madrid na Chelsea kucheza ugenini huko Slovenia na kutoka 1-1 na NK Maribor.

Kwenye Ligi, Wikiendi iliyopita, Liverpool ilichapwa 1-0 na Newcastlle na Chelsea kuifunga QPR Bao 2-1.

Msimu uliopita, kwenye Mechi kama hii, Chelsea iliitwanga Liverpool mabao 2-0.

Ratiba Jumamosi Novemba 8,mechi zote kwa saa za Tanzania.
Liverpool v Chelsea 1545

Burnley v Hull 1800

Man United v Crystal Palace 1800

Southampton v Leicester  1800

West Ham v Aston Villa 1800

QPR v Man City 2030

 
Jumapili Novemba 9

 Sunderland v Everton 1630

Tottenham v Stoke 1630

West Brom v Newcastle 1630

1900 Swansea v Arsenal

0 comments:

Post a Comment