Thursday, 2 April 2015

Kanu asema Supe Eagles si wazuri kwa sasa.


Nyota wa zamani wa klabu ya  Arsenal na timu ya taifa ya Nigeria  Kanu Nwankwo amesisitiza kuwa timu ya taifa ya Nigeria si nzuri ila amesema itakuja kuwa nzuri muda si mrefu.

Nigeria maarufu kwa jina la Super Eagles haipati matokeo mazuri  tokea watwae ubingwa wa Afrika mwaka 2013.

Kanu amesema kuwa kushindwa kufuzu mashindano ya AFCON mwaka 2015 kule Equatorial Guinea si picha nzuri ila anaamini kuwa timu itakuwa nzuri siki zijazo.

Nyota huyo aliyewahi kuzichezea pia  Ajax na  Inter Milan ameongeza kuwa mgogoro wa soka nchini kwao lazima uwekwe wazi ili timu ipate matokeo mazuri.


Kanu  aliyechezea Nigeria mechi  87 tokea  1994 hadi  2011 ameongeza kuwa hafurahishwi na  mgogoro unaoendelea nchini mwake.

0 comments:

Post a Comment