Australia tayari imetua Brazil,ni nchi ya kwanza kufika kabla ya kombe la dunia 2014.
Timu ya taifa ya Australia imekuwa timu ya kwanza kuwasili nchini
Brazil, huku zikisalia siku kumi na nne kabla ya fainali za kombe la
dunia za mwaka 2014 kuanza kutimua vumbi lake kwenye viwanja 12
tofauti,.
Australia wamewasili nchini Brazil katika mji wa Curitiba na watakaa
hapo kwa siku kadhaa, kabla ya kuelekea kwenye mji wa Vitoria ambapo
ndipo mchezo wao wa kwanza wa kundi la pili dhidi ya chile utakapochezwa
July 13.
Socceroos wamewahi kuwasili nchini Brazil kwa lengo la kuendelea na
kambi ya kujiandaa na fainali hizo, na pia watautuimia muda wa majuma
mawili uliosalia kwa lengo la kuizoea hali ya hewa ya kusini mwa bara la
Amerika.
Kiungo wa Socceroos ama timu ya taifa ya Australia Tommy Oar, amesema
wamefurahishwa na mapokezi waliyoyapata kutoka kwa mashabiki
waliojitokeza kuwalaki kwenye uwanja wa ndege wa Southern city, ambapo
wanaamini huenda miongoni mwa mashabiki hao wakawa wafuasi wa
kuwashangilia watakapoanza kampeni ya kuusaka ubingwa wa dunia.

0 comments:
Post a Comment