Sunday, 25 May 2014

Gareth Bale aingia kwenye list ya waingereza waliotwaa mataji ya UEFA

Gareth Bale ameingia kwenye list ya majina ya wachezaji wa kiingereza waliotwa mataji ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya klabu yake ya Real Madrid kushinda mabao  4-1 dhidi ya  Atletico Madrid mchezo uliomalizika kule jijini Lisbon Ureno jumamosi hii;
Diego Godin  aliipa klabu yake uongozi katika dakika ya 36 ya mchezo
Bale alifunga bao ambalo liliwapa nguvu  Madrid katika mchezo huo  baada ya kazi nzuri ya Di Maria kabla ya  Marcelo na  Cristiano Ronaldo kuongeza mabao mengine na kubeba taji ambalo wao wamelipa jina la  La Decima
Kwa maana hiyo  Bale anaungana na akina  Paul Lambert na  Steve McManaman, ambao walishinda mataji miaka ya 2000 baada ya  Madrid kuifunga  Valencia 3-0, katika wachezaji wa kiingereza waliotwaa mataji ya Ulaya na vilabu vya nje.

Kiungo wa zamani wa Manchester United  Owen Hargreaves  ni mchezaji mwingine wa Uingereza aliyeshinda UEFA na vilabu vya nje baada ya kuisaidia  Bayern Munich kutwaa taji dhidi ya Valencia kwa mikwaju ya pelnati mwaka 2001.

0 comments:

Post a Comment