Tuesday, 6 May 2014

Kazimoto awasili nchini tayari kuitumikia Stars



Kiungo mshambuliaji wa timu ya Al Markhiya ya Qatar, Mwinyi Kazimoto amewasili nchini kujiunga na kikosi cha Taifa Stars kinachojiandaa na mechi ya kufuzu michuano ya Afrika dhidi ya Zimbabwe. 
Kazimoto ametua nchini jana ambapo kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho la Soka nchini TFF iliyotumwa leo mchezaji huyo ameshaondoka kwenda Tukuyu, mkoani Mbeya tayari kujiunga na timu hiyo iliyoweka kambi yake huko chini ya kocha Mart Nooij. 
Stars ilicheza mchezo wa kirafiki wa maandalizi dhidi ya Malawi Jumapili iliyopita ambapo walitoka sare ya bila ya kufungana mchezo ambao ulikuwa sehemu ya maandalizi kwa ajili ya mechi hiyo dhidi ya Zimbabwe.

0 comments:

Post a Comment