Kikosi cha Zambia chatajwa kucheza na Japan
Kocha wa timu ya taifa ya Zambia Patrice Beaumelle ametangaza kikosi cha wachezaji ambacho kitacheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Japan siku ya June 6.Beaumelle amewaita wachezaji watatu kutoka kikosi cha vijana chini ya umri wa miaka 20 (U-20) ambacho kiliitoa timu ya Msumbiji katika raundi ya pili ya kufuzu kwenda Senegal kwa michuano ya vijana chini ya umri huo mwaka 2015.
Wachezaji hao ni viungo Lubambo Musonda,mshambuliaji Patrick Ngoma na kipa Mangani Banda.
Pia amewaita Isaac Chansa, Mukuka Mulenga na James Chamanga.
Mchezo huo utachezwa katika mji wa Tampa, Florida katika uwanja wa Raymond James kule Marekani.
Zambia inajiandaa kwa ajili ya kufuzu mataifa Afrika lakini Japana wanatumia mchezo huo kwa ajili ya kuelekea kombe la dunia kule Brazil ambapo wamepangwa sambamba na Colombia, Greece na Ivory Coast katika kundi la C
Kikosi:
Makipa: Kennedy Mweene, Toaster Nsabata, Mangani Banda, Joshua Titima
Walinzi: Davies Nkausu, Jimmy Chisenga, Stoppila Sunzu, Hichani Himonde, Kondwani Mtonga, Joseph Musonda, Emmanuel Mbola, Rodrick Kabwe, Adrian Chama, George Chilufya
Viungo: Nathan Sinkala, Justin Zulu,Isaac Chansa, Chisamba Lungu, Felix Katongo, Christopher Katongo, Fwayo Tembo, Mukuka Mulenga, Lubambo Musonda, Shadreck Malambo, Kennedy Mudenda
Washambuliaji: Jacob Mulenga, Emmanuel Mayuka, Moses Phiri, Ngoma Patrick, James Chamanga

0 comments:
Post a Comment