Kinda wa Uholanzi akiri kuitamani Manchester United,amwambia wakala yu tayari kuondoka.
Winga wa klabu ya PSV Eindhoven Memphis Depay amemwambia wakala wake kuwa yuko tayari kujiunga na Manchester United ambao wameonesha nia ya kumsajili mholanzi huyo.
Kocha mpya wa Manchester United Louis van Gaal ni mshabiki mkubwa wa kijana huyo mwenye miaka 20 na amemtaja katika kikosi cha wachezaji watakaokwenda kombe la dunia nchini Brazil 2014.
Kwa mujibu wa gazeti la Voetbal International, Depay amekubali mwenyewe kujiunga na klabu hiyo baada ya fainali za kombe la dunia.
Van Gaal anamhusudu kinda huyo. Vana Gaal mwenye miaka 62 alichaguliwa kuwa kocha wa Manchester United mapema mwezi huu na amekabidhiwa kiasi cha £200 milion ili asajili.
Masheatani wekundau pia wameelekeza nguvu zao kumsajili winga wa klabu ya Dnipro Yevhen Konoplyanka, ambao wanacheza idara sawa uwanjani na Depay ila Depay anapewa nafasi kubwa ya kujiunga na Manchester.
Van Gaal ambaye anaonekana kutaka kuwasajili wachezaji wengi wa Uholanzi baada ya tamati ya kombe la dunia anataka kuibadilisha klabu akiwa na malengo ya kubeba ubingwa katika msimu wake wa kwanza.
Wachezaji wawili wa Feyenoord Bruno Martins Indi na Jordy Clasie wanatajwa sana kujiunga na klabu hiyo sambamba na Wesley Sneijder pamoja Stefan de Vrij.
Kocha mpya wa Manchester United Louis van Gaal ni mshabiki mkubwa wa kijana huyo mwenye miaka 20 na amemtaja katika kikosi cha wachezaji watakaokwenda kombe la dunia nchini Brazil 2014.
Kwa mujibu wa gazeti la Voetbal International, Depay amekubali mwenyewe kujiunga na klabu hiyo baada ya fainali za kombe la dunia.
Van Gaal anamhusudu kinda huyo. Vana Gaal mwenye miaka 62 alichaguliwa kuwa kocha wa Manchester United mapema mwezi huu na amekabidhiwa kiasi cha £200 milion ili asajili.
Masheatani wekundau pia wameelekeza nguvu zao kumsajili winga wa klabu ya Dnipro Yevhen Konoplyanka, ambao wanacheza idara sawa uwanjani na Depay ila Depay anapewa nafasi kubwa ya kujiunga na Manchester.
Van Gaal ambaye anaonekana kutaka kuwasajili wachezaji wengi wa Uholanzi baada ya tamati ya kombe la dunia anataka kuibadilisha klabu akiwa na malengo ya kubeba ubingwa katika msimu wake wa kwanza.
Wachezaji wawili wa Feyenoord Bruno Martins Indi na Jordy Clasie wanatajwa sana kujiunga na klabu hiyo sambamba na Wesley Sneijder pamoja Stefan de Vrij.
0 comments:
Post a Comment