Kipa wa Arsenal akubali kujiunga na Swansea City, alipangua pelnati 2 kuelekea fainali ya FA
Golkipa wa klabu ya Arsenal Lukasz Fabianski amekubali kujiunga na klabu ya Swansea City pindi mkataba wake utakapomalizika mwezi ujao.
Taarifa iliyoandikwa leo na mtandao wa klabu ya Arsenal ni kwamba kipa huyo amekubali mwenyewe kujiunga na Klabu yake mpya inayotumia uwanja wa the Liberty."Kila mtu ndani ya Arsenal anamshukuru Lukasz kwa mchango wake ndani ya klabu yetu na tunamtakia maisha mema katika timu yake mpya," Imeeleza taarifa ya mtandao wa Arsenal.
Kipa huyo mwenye miaka 29 alijiunga na Arsenal akitokea Legia Warsaw mwaka 2007 na amecheza michezo 78 katika mashindano yote.
Ingawa alionesha kiwango cha hali ya juu katika mafanikio ya Arsenal katika mbio zake za kutwaa kombe la FA msimu huu, Fabianski, aliyeokoa pelnati mbili katika mchezo wa nusu fainali dhidi ya Wigan haikumshawishi Wenger kumtumia sana na badala yake Wojciech Szczesny amebaki kuwa chaguo la kwanza.

0 comments:
Post a Comment