Lambert kujiunga na Liverpool
Liverpool wanakaribia kumnasa mshambuliaji wa Southampton na Uingereza Rickie Lambert kwa Dau linaliodaiwa kuwa Pauni Milioni 4 .
Inatarajiwa Lambert atamaliza kupimwa
Afya yake Jumapili kabla Kikosi cha England hakijaruka kwenda Miami huko
Marekani kupiga Kambi yao ya mwisho kabla kuelekea Brazil kwenye
Fainali za Kombe la Dunia.
Mwezi Januari, Southampton iligomea Ofa
ya West Ham kumnunua Lambert lakini safari hii inaelekea wamekubali mshambuliaji huyo mwenye Miaka 32 kuhama.
Southampton waliikata Ofa ya awali ya
Liverpool kakini sasa mazungumzo baina yao yapo hatua nzuri na
yanaelekea atamalizika kwa kuafikiana.
Lambert alikaa Miaka Mitano huko Anfield
akiwa Chuo cha Soka kabla hajatemwa akiwa na Miaka 15 lakini bado ni
Mpenzi wa Liverpool hadi hii Leo.
Mbali ya Lambert, Liverpool pia
wanaongea na Southampton ili wamchukue Kiungo wao, Adam Lallana, mwenye
Miaka 26, ambae yuko Kikosi cha England hivi sasa.
0 comments:
Post a Comment