Wednesday, 28 May 2014

Malinzi atuma rambirambi msiba wa kocha Mwale



Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amemtumia salamu za rambirambi Rais wa Chama cha Mpira wa Miguu Zambia (FAZ), Kalusha Bwalya kutokana kifo cha Kocha wa timu ya Nkana FC, Masauso Mwale.
Marehemu Masauso Mwale amezikwa jana katika makaburi ya Kansenshi, Ndola ambapo alifariki kwa ajili ya gari Mei 23 akiwa anaelekea kwenye kambi ya klabu ya Nkana ili kujiandaa na mchezo wa kombe la shirikisho barani  Afrika dhidi ya Sewe Sports ya Ivory coast,amefariki akiwa na miaka  51.
Amesema amepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha ghafla cha Kocha Mwale, na kuongeza kuwa msiba huo si pigo kwa Zambia pekee bali Afrika kwa ujumla kwa vile ni mfano wa kuigwa kwa makocha wazalendo waliozipatia mafanikio makubwa klabu za Afrika.
Rais Malinzi amemuomba Rais Bwalya kutuma salamu zake za rambirambi kwa familia ya Mwale, na kuitaka kuwa na moyo wa uvumilivu katika kipindi hiki kigumu cha msiba huo mzito kwao.

0 comments:

Post a Comment