Wednesday, 28 May 2014

Real na Athletico Madrid washitakiwa na UEFA

Shirikisho la soka barani Ulaya UEFA imewafungulia Mashitaka Kocha wa Atletico Madrid Diego Simeone na Kiungo wa Real Madrid Xabi Alonso kwa kuwatuhumu kufanya Utovu wa Nidhamu kwenye Fainali ya ligi hiyo ya mabingwa ulaya  iliyochezwa Jumamosi iliyopita huko Lisbon, Ureno na Real Madrid kuichapa Atletico Madrid mabao 4-1.
Wote hao wawili wameshitakiwa kwa makosa ya kuvamia Uwanja.
Mara mbili Diego Simeone aliingia Uwanjani wakati wa Dakika za Nyongeza 30 kwenda kumkabili Beki wa Real Raphael Varane na ikabidi azuiwe na Wasaidizi wake.
Pia Simeone alionyesha kukasirishwa na Refa Bjorn Kuipers wa Uholanzi.
Nae Xabi Alonso, ambaye alikosa kucheza Fainali hiyo kwa sababu alikuwa Kifungoni, alionekana akikimbia nje ya Uwanja baada ya Mechi hiyo.
UEFA imetamka kuwa Kesi za wawili hao zitasikilizwa hapo Julai 17 na wakipatikana na hatia baadhi ya Adhabu zao ni kuzikosa Mechi za UEFA  Msimu ujao.
Vile vile, UEFA imezifungulia Mashitaka Klabu zote mbili, Real Madrid na Atletico Madrid, kwa kuzoa Kadi za Njano 5 kila moja katika Fainali hiyo.
Kwenye Mechi hiyo, Wachezaji 7 wa Atletico na 5 wa Real walipewa Kadi za Njano.

0 comments:

Post a Comment