Wednesday, 28 May 2014

Van der Vaart nje kombe la dunia

Kocha wa timu ya taifa ya Uholanzi  Louis van Gaal  atakuwa na kikosi chake  bila kupata huduma ya mchezaji   Rafael van der Vaart katika fainali za kombe la dunia Brazil mwaka 2014 baada ya kuumia  msuli wa nyama  nyuma ya goti yaani Calf.
Taarifa iliyoandikwa katika mtandao wa goal.com ni kwamba Van der Vaart  aliumia wakati akifanya mazoezi jana siku ya jumanne katika kambi ya timu hiyo iliyopo nchini Ureno na kwa sasa ametolewa kwenye kikosi hicho kitakachokwenda Brazil.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 alikuwa anasubiri kikosi cha mwisho cha wachezaji  23 wa Uholanzi  kitajwe ambacho kitakwenda Brazil lakini kutokana na matatizo ya kimwili atakosa fainali yake ya tatu za kombe la dunia tokea aanze kucheza soka baada ya mwaka  2006 na 2010 kucheza fainali hizo.

0 comments:

Post a Comment