Monday, 26 May 2014

Ronaldo amfunika Messi bado kidogo kwa Raul

Mchezaji bora wa dunia na klabu ya Real Madrid Cristiano Ronaldo  Amempita nyota wa Barcelona  Lionel Messi  katika rekodi za ufungaji mabao katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Ulaya baada ya kufunga bao jumamosi hii kwenye fainali ya UCL dhidi ya Athletico Madrid kule Lisbon.
Ronaldo mwenye miaka  29 ambaye alibeba tuza ya  Ballon d'Or mwezi January kutoka kwa Messi, alifunga bao la nne kwa njia ya pelnati katika ushindi wa mabao 4-1 kule Lisbon.
Ronaldo kwa sasa ameachwa mabao matatu na mchezaji wa zamani wa  Madrid  Raul, ambaye amefunga mabao 71 katika michezo 144 ya ligi ya mabingwa ulaya.

Mreno huyo hana uwiano mzuri wa kuifungia mabao Madrid kwa sasa amefunga mabao 68 katika michezo 107 huku Messi akifunga mabao 67 katika michezo 86 ya ligi hiyo ya mabingwa ambapo mabingwa wapya kwa msimu huu ni Real Madrid.

Rekodi za ufungaji mabao Uefa
Mchezaji                  Mabao       Michezo
Raul                          71               144
Christian Ronaldo     68              107
Messi                         67              86
Van Nistelrooy          60              81
Shevchenko               59              116

0 comments:

Post a Comment