Thursday, 22 May 2014

Wambura mwanachama halali wa Simba-Rage.

MWENYEKITI wa Simba anayemaliza muda wake, Ismail Aden Rage, amewaonya wanachama kuwa makini kuelekea uchaguzi mkuu, kwani kitendo cha kupandikiza maneno kwa Mgombea wa Urais Michael Wambura kitaharibu mchakato mzima wa uchaguzi.
Uchaguzi Mkuu wa Simba unatarajia kufanyika Juni 29 mwaka huu, huku leo ikiwa ni siku ya mwisho kuwasilisha pingamizi kuelekea usaili unaotarajiwa kufanyika Mei 29 Bwalo la Maofisa wa Polisi Oysterbay.
Akizungumzia hilo, Rage alisema, wapo wanachama wanasema Wambura sio mwanachama kitendo ambacho sio kweli, huku akidai kuwa, katika kila jambo kuna taratibu za kufuata na kuwataka wanachama kulitambua hilo.
Aidha, Rage alisema, mbali na hilo, pia endapo watafanya hivyo kutaka kumuengua Wambura kwa kutofuata taratibu, itawasababishia wao kupata viongozi wabovu katika uchaguzi huo.
“Wapo wanaotaka Wambura afukuzwe uanachama, wengine wanasema sio mwanachama, mpaka kufikia uamuzi huo kuna taratibu za kufuata ikiwemo ya kumpa nafasi ya kusikilizwa, vinginevyo wataharibu uchaguzi au watajikuta wanapata viongozi wabovu,” alisema Rage na kuongeza.
Nipo Dodoma, nafuatilia kwa karibu sana mchakato huu wa uchaguzi, wapo wanaosema Wambura aenguliwe kwa sababu alienda mahamani, wengine wanasema asigombee kwa sababu alishawahi kufukuzwa uanachama, mimi nimeongoza vikao vyote vya Simba, sijawahi kuona Wambura anafukuzwa, au anavuliwa uanachama, hiyo sio kweli kabisa,” alisema Rage.
Aliongeza kwa kuwaasa Simba kuwa makini na uchaguzi huo, kwani kama wanataka kumuengua Wambura kuna taratibu za kufuata na lazima wampe haki ya kusikilizwa.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

Post a Comment