Monday, 2 June 2014

David Villa atua rasmi katika ligi ya MLS

Klabu ya New York City FC imethibitisha rasmi kuwa Mhispania ambaye anaongoza kwa kuifungia timu ya taifa mabao mengi  David Villa amekuwa mchezaji wao wa kwanza Kusajiliwa katika ligi ya Marekani  MLS.

Mshambuliaji huyo wa zamani wa  Valencia na  Barcelona anaondoka Atletico Madrid baada ya kutumikia msimu moja na kufunga mabao  13 na kuisaidi klabu yake kufika fainali ya ligi ya mabingwa Ulaya tokea mwaka 1996.

 “Siku zote katika kipaji changu najaribu kitu kipya na hii inaonesha kitu muhimu kwangu ”, Villa mwenye miaka 32 aliliambia mtandao wa New York City.

“Ninataka kuisaidia  MLS iendelea kukua kwa kucheza,kufunga mabao na pia kuifanya  New York City FC iwe klabu bora katika ligi hii.'alisema Villa
Villa ameichezea Hispania michezo  94 , amefunga mabao  56 na ametajwa katika kikosi cha wachezaji 23 kwenda katika kombe la dunia nchini Brazil.

0 comments:

Post a Comment