Wednesday, 11 June 2014

Imekula kwa Manchester United,Muller ajifunga Munich Hadi 2019

Muller na Lahm
Wachezaji Philipp Lahm  na  Thomas Muller  wameongeza  mkataba wa miaka miwili wa kuitumikia klabu yao ya Bayern Munich.

Nahodha Lahm kwa sasa atawatumikia mabingwa wa  Bundesliga  hadi June 2018, wakati  Muller - ambaye alikuwa akitajwa kuondoka atabaki Allianz Arena  hadi  June 2019.
Hayo yameelezwa na mkurugenzi mtendaji wa klabu  Karl-Heinz Rummenigge.
"Philipp Lahm na Thomas Muller  ni watu muhimu sana ndani ya FC Bayern," Rummenigge alisema hayo kupitia mtandao wa klabu.
"Wamekuwa waaminifu kwa klabu yetu tokea waanze kucheza na bado tuna malengo ya baadaye na hawa vijana.
 Lahm alijiunga na  Bayern akiwa na umri wa miaka 11 na inawezekana akamaliza kipaji chake kwa kuitumikia Bayern .
Alipoulizwa kuhusu mkataba huo Lahm alieleza kuwa anafuraha zaidi kwa kuendelea kuitumikia klabu na kumaliza kipaji chake Alianz Arena
Muller alikuwa anazungumziwa  sana kuwakacha  Bavaria,  ili ajiunge na  Manchester United chini ya kocha wake wa zamani Louis van Gaal
Kwa maana hiyo sasa wachezaji ambao walitakiwa na Van Gaal akina Robben,Muller na Kroos wameota mbaya ndani ya Old Traford.
Muller mwenye miaka 24 amesema kuwa taarifa zote zilizosemwa kuhusu yeye sasa zimefika mwisho na yuko tayari kuitumikia klabu yake.

Lahm na Muller  kwa sasa wapo Brazil kujiandaa na michezo ya kombe la dunia ambayo itaanza kesho na wana nafasi ndani ya kikosi cha kwanza cha  kocha  Joachim Low.

0 comments:

Post a Comment